Philipo Mrutu ni mtaalamu wa kilimo na biashara ya kilimo kutoka wilaya ya Morogoro nchini Tanzania. Anasema kuwa faida za kulima mazao mbalimbali katika shamba moja ni kwamba ardhi inatumika vizuri na mazao yanasaidiana au kutegemeana.
Anaongeza: “Pia inasaidia kuongeza rutuba, kwa mfano mtu anapolima na kuchunga kwa wakati mmoja, mabaki ya chakula cha mifugo yanayotumika katika kilimo tayari yana rutuba, ambayo inaweza kusaidia kilimo kustawi.
Bw. Mrutu anabainisha kuwa mazao mchanganyiko yanasaidia kutunza unyevu wa udongo na miti ikipandwa pembezoni mwa bwawa inatoa kivuli na kuboresha hali ya hewa hasa katika kipindi cha kiangazi ambacho dunia inakabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa.
Bwana Njelekela anasema kilimo mseto kimemsaidia kwa njia nyingi. Anafafanua: “Nawashauri wakulima wa eneo langu kuanza kulima mseto kwasababu kwangu nimeona faida nyingi ikiwamo mapato bora. Ninaweza kutunza familia yangu kwa sababu ya kupanda mseto.”
Chanzo:
https://wire.farmradio.fm/farmer-stories/tanzania-intercropping-boosts-farmer-incomes/